41. Yesu Aliniita

Yesu aliniita, “njoo,
Raha iko kwangu,
Kichwa chako ukilaze
Kifuani mwangu.”

Nilikwenda kwake mara,
Sana nilichoka;
Nikapata kwake raha,
Na furaha tena.

Yesu aliniita, “njoo,
Kwangu kuna maji,
Maji ya uzima, bure,
Unywe uwe hai, ”

Nilikwenda kwake mara
Na maji nikanywa:
Naishi kwake, na kiu
Kamwe sina tena.

Yesu aliniita, “njoo,
Dunia ni giza,
Ukinitazama nuru
Takung’arizia.”

Nilikwenda kwake mara
Yeye jua langu,
Ni kila wakati mwanga
Safarini mwangu.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top