86.Damu Imebubujika

There is a fountain filled with blood

1.
Damu imebubujika,
Ni ya Imanueli,
Wakioga wenye taka
Husafiwa kweli.

2.
Ilimpa kushukuru
Mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru,
Yanioshe ndani.

3.
Kondoo wa kuawa,
Damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa
Kwa utimilivu.

4.
Bwana, tangu damu yako
Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako;
Taimba milele.

5.
Nikifa lazidi kwimba
Sifa za wokovu,
Ulini ujaponyamaa
Vumbini mwa ufu.

6.
Bwana, umenikirimu,
Nisiyestahili,
Kwa damu yako, sehemu
Ya mali ya kweli.

7.
Nikubali kukwimbia,
Mbinguni milele,
Mungu nitakusifia
Jina lako pweke.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top