11.Nina haja nawe

Nina haja nawe
Kila saa;
Hawezi mwingine
Kunifaa.

Yesu, nakuhitaji
Vivyo kila saa!
Niwezeshe, Mwokozi,
Nakujia.

Nina haja nawe;
Kaa nami,
Na maonjo haya,
Hayaumi.

Nina haja nawe;
Kila hali,
Maisha ni bure,
Uli mbali.

Nina haja nawe,
Nifundishe
Na ahadi zako
Zifikishe.

Nina haja nawe,
Mweza yote,
Ni wako kabisa
Siku zote.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top