Ewe Roho wa Mbinguni
Uje kwetu sasa.
Ufanye makazi yako
Ndani ya Kanisa.
Uje kwetu sasa.
Ufanye makazi yako
Ndani ya Kanisa.
Ndiwe mwanga, umulike
Tupate jikana;
Mengi kwetu yapunguka,
Tujalize, Bwana.
Ndiwe Moto, teketeza
Taka zetu zote:
Moyo na iwe sadaka
Ya Mwokozi, yote.
Ndiwe Umande, na kwako
Tutaburudika,
Nchi kavu itakuwa
Ni yenye Baraka.
Roho wa Mbinguni uwe
Nasi hapa chini,
Mwili uufananishe
Na kichwa Mbinguni.