Jesus, our blessed Lord, will come
1.
Bwana Yesu atakuja, Vumilia!
Omba, ukiwa na haja, Vumilia!
Mbinguni Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako,
Nawe utafika huko, Vumilia!
Omba, ukiwa na haja, Vumilia!
Mbinguni Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako,
Nawe utafika huko, Vumilia!
2.
Ikikucheka dunia, Vumilia!
Mwovu atakuvizia, Vumilia!
Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda
Roho yako akupenda, Vumilia!
Mwovu atakuvizia, Vumilia!
Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda
Roho yako akupenda, Vumilia!
3.
Na ukiwa hatarini, Vumilia!
Dhiki nyingi duniani, Vumilia!
Vyatupasa kuyakuta, Majaribu na matata.
Na Bwana hakutuficha, Vumilia!
Dhiki nyingi duniani, Vumilia!
Vyatupasa kuyakuta, Majaribu na matata.
Na Bwana hakutuficha, Vumilia!
4.
Adui wakikutana, Vumilia!
Na ndungu wakikukana, Vumilia!
Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutisha
Mungu chini atashusha; Vumilia!
Na ndungu wakikukana, Vumilia!
Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutisha
Mungu chini atashusha; Vumilia!
5.
Moyoni una majonzi, Vumilia!
Ndiyo bonde-ya-machozi Vumilia!
Hima, tutaandamana Kwetu Mbinguni na Bwana,
Tena hatutaachana; Vumilia!
Ndiyo bonde-ya-machozi Vumilia!
Hima, tutaandamana Kwetu Mbinguni na Bwana,
Tena hatutaachana; Vumilia!