Ten thousand times ten thousand
1.
Maelfu na maelfu,
Wenye nguo bora!
Masafu ya waongofu
Wenye na bendera!
Amekwisha kamili
Vita vya Shetani
Fungueni lango hili;
Njooni, ingieni!
2.
Imbeni aleluya,
Zipae Mbinguni!
Pigeni sana sauti
Kwa kutumaini!
Kwa hiyo vilumbwa
Nchi hata Mbingu
Dhiki za muda zikisha,
Asifiwe Yesu.
3.
Loo! Tukionana
Pwani ya ng’ambo!
Loo! Tukishirikiana
Milele Mbinguni!
Midomo yote pia
Huko itaimba
Wajane kufufukiwa
Na kila yatima!
4.
Himiza enzi yako,
Uliye fufuka,
Utimize watu wako,
Wakosaji pia,
Mpendwa wa taifa
Twakutumaini!
Uzifunue ishara
Urudi enzini!