New every morning is the love
1.
Mapya ni mapenzi hayo,
Asubuhi tuonayo,
Saa za giza hulindwa,
Kwa uzima kuamshwa.
Asubuhi tuonayo,
Saa za giza hulindwa,
Kwa uzima kuamshwa.
2.
Kila siku, mapya pia,
Rehema, wema, na afya,
Wokovu, na msamaha,
Mawazo mema, furaha.
Rehema, wema, na afya,
Wokovu, na msamaha,
Mawazo mema, furaha.
3.
Tukijitahidi leo
Na mwendo utupasao,
Mungu atatueleza
Yatakayompendeza.
Na mwendo utupasao,
Mungu atatueleza
Yatakayompendeza.
4.
Mambo yetu ya dunia
Mungu atayang’aria.
Matata atageuza
Yawe kwetu ya baraka.
Mungu atayang’aria.
Matata atageuza
Yawe kwetu ya baraka.
5.
Yaliyo madogo, haya
Mungu tukimfanyia,
Yatosha: tutafaidi
Huvuta kwake zaidi.
Mungu tukimfanyia,
Yatosha: tutafaidi
Huvuta kwake zaidi.
6.
Ewe Bwana, siku zote,
Tusaidie kwa yote:
Mwendo wetu wote vivyo,
Uwe kama tuombavyo.
Tusaidie kwa yote:
Mwendo wetu wote vivyo,
Uwe kama tuombavyo.