1.
Dhambi ikikulemea,
Kwa Bwana rehema;
Hivi sasa tegemea
Neno la salama.
Chorus:
Tegemea, tegemea,
Akwita sasa.
Ni Mwokozi, ni
Mwokozi; amini sasa.
2.
Yesu amemwaga damu
Ya nyingi baraka;
Nawe sasa oga mumu
Zioshwamo taka.
3.
Ni njia yeye hakika
Hwongoza rahani;
Usikawe kumshika,
Uwe barakani.
4.
Karibu nawe wingie
Mwetu safarini,
Twende tukamwamkie,
Milele Mbinguni.