103. Kaa Nami

Abide with me

1.
Kaa nami, ni usiku tena;
Usiniache gizani, Bwana;
Msaada wako haukomi;
Nili peke yangu, kaa nami.

2.
Siku zetu hazikawi kwisha.
Sioni la kunifurahisha;
Hakuna ambacho hakikomi,
Usiye na mwisho, kaa nami.

3.
Nina haja nawe kila saa;
Sina mwingine wa kunifaa;
Mimi nitaongozwa na nani
Ila Wewe Bwana, kaa nami.

4.
Sichi neno uwapo karibu;
Nipatalo lote, si taabu;
Kifo na kaburi haviumi;
Nitashinda kwako, kaa nami.

5.
Nilalapo nikuone wewe,
Gizani mote nimulikiwe;
Nuru za mbinguni hazikomi
Siku zangu zote kaa nami.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top