37.Waitwa, Mwovu, na Bwana

Beulah Land

1.
Waitwa, mwovu, na Bwana
Umwendee hima sana,
Usafiwe dhambi zako,
Humwoni ni mwema wako?

Chorus:
Unaitwa! Itika tu!
Umwendee Bwana Yesu!
Sifiche makosa yako,
Uungame dhambi zako!
Kristo tu umuamini,
Ndiyo njia ua Mbinguni.

2.
Alilipa damu yake
Ili kukukweza kwake;
Alikufa yeye Bwana,
Mimi nawe tuwe wema.

3.
Ukifanywa kuwa mwema
Mwishoni utasimama,
Utaingia rahani
Na wapenzi wa zamani.

4.
Ni mwanga tu, nchi ile;
Uovu hauko kule,
Kwamba wataka ufike
Sharti huku uosheke.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top