9.Yesu kwetu ni rafiki

What a Friend we have in Jesus

1.
Yesu kwetu ni rafiki,
Hwambiwa haja pia;
Tukiomba kwa Babaye
Maombi asikia;
Lakini twajikosesha,
Twajitweka vibaya;
Kwamba tulimwomba Mungu
Dua angesikia.

2.
Una dhiki na maonjo?
Una mashaka pia?
Haifai kufa moyo,
Dua atasikia
Hakuna mwingine mwema
Wa kutuhurumia;
Atujua tu dhaifu;
Maombi asikia.

3.
Je, hunayo hata nguvu,
Huwezi kuendelea,
Ujapodharauliwa
Ujaporushwa pia,
Watu wange kudharau,
Wapendao dunia,
Hukwambata mikononi,
Dua atasikia.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top