132. Sauti Sikilizeni

Hark the sound of holy voices

1.
Sauti sikilizeni
Za waimbao juu
“Aleluya, Aleluya,
Aleluya, Mkuu!”
Wako makundi-makundi
Kama nyota wang’ara,
Kwa makuti ya mitende,
Na meupe wamevaa.

2.
Wazazi na manabii
Wafanyaji wa njia;
Mashahidi, waandishi,
Nao wafalme pia!
Mabikira, kina-mama,
Wajane wa kusali,
Waimba wakikutana
“Msifu Imanweli.”

3.
Watu toka huzunini
Wameosha na nguo,
Ni kwa damu yake Yesu,
Maonjo, mbali nao!
Walitekwa, wakikatwa
Hata kwa misumeno,
Kwao kifo na Shetani
Walishindiwa mno.

4.
Mungu mumo mwake
Mungu,
Nuru mumu mwa nuru,
Kwa kufungamana mwako
Tutaishi mahuru;
Tujalize, Imanweli,
Kujaa kwako Wewe
Mungu Baba, Mungu
Mwana,
Mungu Roho, tunawe.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top