Not all the blood of beasts
1.
Kwa wingi wa nyama,
Na sadaka pia,
Hupata wapi salama,
Kwondoa hatia?
2.
Sadaka ni Yesu,
Hwondoa makosa;
Dhabihu mwenye jina kuu,
Atanitakasa.
3.
Kwa yangu imani
Nikuweke sasa;
Mkono mwako kichwani
Kukiri makosa.
4.
Roho yakumbuka
Mambo ya Mtini,
Mzigo ulijitweka,
Ndiyo yangu deni.
5.
Deni hutanguka,
Tukimuamini;
Kwa damu tumeokoka
Twimbe furahani.