83.Kwa Wingi Wa Nyama

Not all the blood of beasts

1.
Kwa wingi wa nyama,
Na sadaka pia,
Hupata wapi salama,
Kwondoa hatia?

2.
Sadaka ni Yesu,
Hwondoa makosa;
Dhabihu mwenye jina kuu,
Atanitakasa.

3.
Kwa yangu imani
Nikuweke sasa;
Mkono mwako kichwani
Kukiri makosa.

4.
Roho yakumbuka
Mambo ya Mtini,
Mzigo ulijitweka,
Ndiyo yangu deni.

5.
Deni hutanguka,
Tukimuamini;
Kwa damu tumeokoka
Twimbe furahani.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top