61.Tumesikia Mbiu

Tumesikia mbiu:
Yesu lo! aponya,
Utangazeni kote,
Yesu, lo! aponya.
Tiini amri hiyo;
Nchini na baharini,
Enezeni mbiu hii;
Yesu , lo! aponya.

Imbeni na vitani;
Yesu, lo! aponya;
Kwa nguvu ya kombozi,
Yesu, lo! aponya.
Imbeni wenye shida,
Unapoumwa moyo.
Na karibuni imba;
Yesu, lo! aponya.

Mawimbini uenee;
Yesu, lo! Aponya;
Wenye dhambi jueni;
Yesu, lo! Aponya.
Visiwa na viimbe,
Vilindi itikeni,
Na nchi shangilieni;
Yesu, lo! Aponya.

Upepo utangaze;
Yesu, lo! Aponya;
Mataifa yashangaaa;
Yesu lo! Aponya.
Milimani, bondeni,
Sauti isikike
Ya wimbo wa ushindi;
Yesu, lo! Aponya.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top