82.Sioni haya kwa Bwana

At the Cross

1.
Sioni haya kwa Bwana
Kwake nitang’ara!
Mti wake sitakana
Ni neno imara!

Chorus
Msalaba ndio asili ya mema,
Nikatua mzigo hapo;
Nina uzima, furaha daima,
Njioni kufurahini papo.

2.
Kama kiti chake vivyo
Ni yake ahadi;
Aliyowekewa navyo
Kamwe, havirudi.

3.
Bwana wangu, tena Mungu,
Ndilo lake jina!
Hataacha roho yangu
Wala kunikana.

4.
Atakiri langu jina
Mbele za Babaye,
Anipe pahali tena
Mbinguni nikae.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top