1.
Yesu zama Bethlehemu,
Aliyezaliwa kwa aibu,
Ndiye mwakozi wa ulimwengu,
Akaja kwa mimi.
Chorus:
Akaja kwa mimi; akaja kwa mimi;
Ndiye mwaokozi wa ulimwengu,
Akaja kwa mimi.
2.
Yesu akafa msalabani,
Kuniponya akalipa deni,
Ni la ajabu ya jinsi gani
Kunifia mimi!
Chorus:
Kunifia mimi! Kunifia mimi!
Ni la ajabu ya jinsi gani
Kunifia mimi.
3.
Ni yeye huyo tangu asili;
Na nilipotanga-tanga mbali
Alikuja kwa upole, kweli
Kuniita mimi.
Chorus:
Kuniita mimi; Kuniita mimi;
Alikuja kwa upole, kweli
Kuniita mimi.
4.
Yesu Kristo atarudi tena,
Hilo lanifurahisha sana.
Yeye Bwana akionekana
Kunijia mimi.
Chorus:
Kunijia mimi, kunijia mimi,
Yeye Bwana akionekana
Kunijia mimi.