73.Yesu Zamani Bethlehemu

Jesus my Saviour, to Bethlehem came

1.
Yesu zamani Bethilehemu
Aliyezaliwa kwa aibu,
Ndiye Mwokozi wa ulimwengu,
Akaja kwa mimi.

Chorus
Akaja kwa mimi; akaja kwa mimi;
Ndiye Mwokozi wa ulimwengu,
Akaja kwa mimi.

2.
Yesu akafa Msalabani,
Kuniponya akalipa deni;
Ni la ajabu ya jinsi gani
Kunifa mimi!

Chorus
Kunifa mimi! kunifa mimi!
Ni la ajabu ya jinsi gani
Kunifa mimi.

3.
Ni Yeye Huyo tangu asili;
Na nilipolanga tanga mbali,
Alikuja kwa upole, kweli
Kuniita mimi.

Chorus
Kuniita mimi;
Alikuja kwa upole, kweli
Kuniita mimi.

4.
Yesu Kristo atarudi tena,
Hilo lanifurahisha sana,
Yeye Bwana akionekana
Kunijia mimi.

Chorus
Kunijia mimi; kunitwaa mimi;
Yeye Bwana akionekana
Kunijia mimi.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top