Tumrudie Bwana
1.
Mbona washangaa njiani?
Mbona warejea nyuma?
Warudi tena gizani,
Alimokutoa Bwana?
2.
Ni ya bure yote haya
Uliyofunzwa ya Mungu?
Ni bure amekufia
Bwana Yesu kwa uchungu?
3.
Wamtia Kristo aibu
Na maneno yake pia?
Siku yaja ya hesabu,
Utamjibuaje Bwana.
4.
Upandayo tena hayo
Halafu utayavuna.
Rudi kwa Bwana upesi;
Mwombe akupokee tena.