58.Mwamba Wenye Imara

Rock of Ages, cleft for me

1.
Mwamba wenye imara,
Kwako nitajificha!
Maji hayo na damu
Yaliyotoka humu,
Hunisafi na dhambi,
Hunifanya mshindi.

2.
Kwa kazi zote pia,
Sitimizi sharia.
Nijapofanya bidii,
Nikilia na kudhii,
Hayaishi makosa;
Ndiwe wa kuokoa.

3.
Sina cha mkononi,
Naja Msalabani;
Nili tupu, nivike;
Ni mnyonge, nishike;
Nili mchafu naja,
Nioshe nisijafa.

4.
Nikungojapo chini,
Nakwenda kaburini;
Nipaapo Mbinguni,
Na kukuona enzini:
Roho yangu na iwe
Rahani mwako wewe.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top