87.Deni Ya Dhambi Ilimalizika

Jesus paid it all

1.
Deni yangu ya dhambi,
Yesu amelipa,
Kwake Msalabani
Nilipewa uzima.

Chorus
Deni ya dhambi,
Msalabani
Ilimalizika,
Ni huru kabisa.

2.
Bwana Yesu asema,
“Mwanangu dhaifu,
Uwezo na ushindi
Hupatikana kwangu.”

3.
Bwana, kweli naona,
Nguvu zako pekee
Huondoa ukoma,
Niwe kipya kiumbe.

4.
Sina wema moyoni,
Nidai neema,
Nakubali kabisa,
Kwa damu kusafiwa.

5.
Hata huko Mbinguni,
Miguu ni pake,
“Yesu alinishia,”
Nitaimba milele.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top