“Man of sorrows,” what a name
1.
Ni “Mtu wa Simanzi,”
Mwana wa Mwenye enzi,
Mwenye mengi mapenzi!
Asifiwe Bwana Yesu!
2.
Akawa Matesoni,
“Mungu Mwana” yakini,
Akatoka Mbinguni;
Asifiwe Bwana Yesu!
3.
Akapata dhihaka,
Mzoea mashaka,
Ndiye yetu sadaka;
Asifiwe Bwana Yesu!
4.
Tu wenye dhambi sana,
Kwake dhambi hamna,
Na Mungu twapatana;
Asifiwe Bwana Yesu!
5.
Alikufa Mtini,
Akalia dhikini,
Sasa yuko Mbinguni;
Asifiwe Bwana Yesu!
6.
Punde atarejea,
Yesu kutunyakua,
Ndipo tutamwimbia;
Asifiwe Bwana Yesu!