85.Ni “Mtu Wa Simanzi

“Man of sorrows,” what a name

1.
Ni “Mtu wa Simanzi,”
Mwana wa Mwenye enzi,
Mwenye mengi mapenzi!
Asifiwe Bwana Yesu!

2.
Akawa Matesoni,
“Mungu Mwana” yakini,
Akatoka Mbinguni;
Asifiwe Bwana Yesu!

3.
Akapata dhihaka,
Mzoea mashaka,
Ndiye yetu sadaka;
Asifiwe Bwana Yesu!

4.
Tu wenye dhambi sana,
Kwake dhambi hamna,
Na Mungu twapatana;
Asifiwe Bwana Yesu!

5.
Alikufa Mtini,
Akalia dhikini,
Sasa yuko Mbinguni;
Asifiwe Bwana Yesu!

6.
Punde atarejea,
Yesu kutunyakua,
Ndipo tutamwimbia;
Asifiwe Bwana Yesu!

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top