83.Kwa Wingi Wa Nyama

Kwa wingi wa nyama,
Na sadaka pia,
Hupata wapi salama,
Kwondoa hatia?

Sadaka ni Yesu,
Hwondoa makosa;
Dhabihu mwenye jina kuu,
Atanitakasa.

Kwa yangu imani,
Nikuweke sasa
Mkono mwako kichwani
Kukiri makosa.

Roho yakumbuka
Mambo ya mtini,
Mzigo ulijitweka,
Ndiyo yangu deni.

Deni hutanguka,
Tukimuamini;
Kwa damu tumeokoka,
Twimbe furahani.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top