Beneath the Cross of Jesus
1.
Chini ya Msalaba
Nalaka simama,
Ndio mwamba safarini,
Wa kivuli chema.
2.
Hapa ni pema sana,
Ni ngome kamili;
Hapa yameonekana,
Mapenzi ya kweli;
Kama alivyoonyeshwa
Yakobo zamani,
Msalaba umekuwa
Ngazi ya Mbinguni.
3.
Na Yesu Msalabani
Walinikemea;
Alikufa niokoke,
Niliepotea;
Naona ajabu sana
Ya mambo make,
Jinsi alivyonipenda,
Nisiyestahili.
4.
Atakayeonana
Na Yesu Mbinguni,
Njia yake aanzapo
Ni Msalabani;
Wokovu upo hapa tu,
Mwingine hapana,
Kisha kuna furaha kuu
Pamoja na Bwana.