O come, all ye faithful
1.
Njoni na furaha, enyi wa imani,
Njoni Bethilehemu upesi!
Amezaliwa jumbe wa Mbinguni;
Njoni tumuabudu, njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.
2.
Mungu wa waungu, Mwanga wa mianga,
Amekuwa radhi kuzaliwa;
Mungu wa kweli, wala si kiumbe;
Njoni tumuabudu, njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.
3.
Jeshi la Mbinguni, imbeni kwa nguvu!
Mbingu zote na zijae sifa!
Sifuni Mungu aliye Mbinguni;
Njoni tumuabudu, njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.
4.
Ewe Bwana Mwema, twakubarikia,
Yesu, utukufu uwe wako;
Neno la Baba limekuwa mwili;
Njoni tumuabudu, njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.