Hark, the herald angels sing
1.
Waimba, sikizeni,
Malaika Mbinguni;
Wimbo wa tamu sana
Wa pendo zake Bwana;
Duniani salama,
Kwa wakosa rehema.
Sisi sote na twimbe
Nao wale wajumbe;
Waimba, sikizeni,
Malaika Mbinguni.
2.
Ndiye Bwana wa Mbinguni,
Tangu milele Mungu,
Amezaliwa mwili,
Mwana wa mwanamwali;
Ametoka enzini,
Kuja ulimwenguni,
Mwokozi atufie,
Ili tupolee.
Waimba, sikizeni,
Malaika Mbinguni.
3.
Mtukufu wa amani
Ametoka Mbinguni,
Jua la haki, ndiye
Atumulikiaye;
Amejivua enzi,
Aliyo ra mapenzi,
Ataka kutuponya,
Kutuzalisha upya.
Waimba, sikizeni,
Malaika Mbinguni.
4.
Njoo upesi, Bwana,
Twakutamani sana;
Kaa nasi, Mwokozi,
Vita hatuviwezi;
Vunja kichwa cha nyoka,
Sura zako andika,
Tufanane na Wewe,
Kwetu sifa upewe.
Waimba, sikizeni,
Malaika Mbinguni.