7.Ni Tabibu Wa Karibu

1.
Ni tabibu wa karibu;
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima;
Ni dawa yake njema.

Chorus:
Imbeni, malaika,
Sifa za Yesu Bwana;
Pweke limetukuka
Jina lake Yesu.

2.
Hatufai kuwa hai,
Wala hatutumai,
Ila kweli yeye ndiye
Atupumzishaye.

3.
Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia;
Twendeni na amani
Hata kwake Mbinguni.

4.
Huliona tamu jina
La Yesu Kristo Bwana,
Yuna sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa.

5.
Kila mume asimame,
Sifa zake zivume;
Wanawake na washike
Kusifu jina lake.

6.
Na vijana wote tena,
Wapendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top