65.Safari

1.
Katika safari yetu
Kwenda Mbinguni
Tusiishe siku zetu
Usingizini.

Chorus
Ng’oani! Tujifungeni,
Twende zetu juu!
Kristo ndiye kiongozi;
Tusihofu tu.

3.
Atwekwe badala yetu,
Mwenyewe Bwana;
Yesu kiongozi wetu
Atapokea.

4.
Kisimani, maji tele,
Maji mazima!
Maji hayo,
Ya milele
Yana neema.

5.
Njiani miiba mingi,
Yatuumiza;
Hofu na hatari nyingi,
Sana zakaza.

6.
Kweli, njia ya Mbinguni
Ni ya mashaka;
Tuwe na Yesu njiani,
Mara hufika.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top