6.Baba, Mwana, Roho

Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi,
Kila tukiamka tunakuabudu
Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi,
Ewe Utatu, tunakusifu.

Baba, Mwana, Roho, wakuaminio
Wanakutolea shukrani zao
Wanakusujudia malaika nao:
Wewe u mwanzo, nawe u mwisho.

Baba, Mwana, Roho, sisi tu gizani,
Utukufu wako hatuoni kosa;
U Mtakatifu, nawe u mapenzi,
U peke yako, mwenzio huna.

Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi,
Ulivyoviumba vyote vyakusifu:
Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi
Ewe Utatu, tunakusifu.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top