59.Peleleza Ndani Yangu

Peleleza ndani yangu,
Iwe safi nia,
Kwangu kama kwako Mungu,
Idhihiri pia.

Peleleza moyo wangu
Uunifunulie,
Yaliyomo ndani yangu
Nami niyajue.

Kwanza washe zako tambi,
Kumefunga giza;
Nijue ambavyo dhambi
Ni la kuchukiza.

Peleleza na mawazo
Ni mbegu za mambo,
Asili ya machukizo,
Maumbuo – umbo.

Zidi kuyapeleleza
Katikati yangu
Hata wishe nifundisha
Udhaifu wangu.

Hapo nikikwinamia
Mbele zako, Mungu,
Hakika nitakujua
U mpenzi wangu.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top