Just as I am without one plea
1.
Nitwae hivi nilivyo,
Umemwaga damu yako,
Nawe ulivyoniita,
Bwana Yesu, naja, naja.
2.
Hivi nilivyo; si langu
Kujiosha roho yangu;
Nisamehe dhambi zangu,
Bwana Yesu, naja, naja.
3.
Hivi nilivyo; sioni
Kamwe furaha moyoni;
Daima ni mashakani,
Bwana Yesu, naja, naja.
4.
Hivi nilivyo kipofu,
Maskini na mpungufu;
Wewe u mtimilifu;
Bwana Yesu, naja, naja.
5.
Nawe hivi utanitwaa;
Nisithubutu kukawa,
Na wewe hutanikataa,
Bwana Yesu, naja, naja.
6.
Hivi nilivyo; mapenzi
Yamenipa njia wazi;
Hali na mali sisazi,
Bwana Yesu, naja, naja.