48.Naweka Dhambi Zangu

I lay my sins on Jesus

1.
Naweka dhambi zangu
Juu yake Bwana,
Kuziondoa, kwangu
Hulemea sana;
Na uaili wangu
Ameuondoa;
Dawa yangu ni damu,
Kwa hiyo napoa.

2.
Na uhitaji wangu
Nitajuvisa
Kwa upungufu wangu
Yeye anatosha;
Majonzi yangu yote
Na mizigo yangu,
Atachukua vyote
Yesu Bwana wangu.

3.
Na roho yangu nayo,
Imechoka sana;
Namletea hiyo
Ilindwe na Bwana;
Ni jema jina lake,
Nalo lapendeza,
Imanweli na kwake
Tutalitukuza.

4.
Natamani daima
Niwe kama Bwana,
Mpole, tena mwema,
Wa mapenzi sana;
Zaidi natamani
Kwenda kwake juu,
Nikaone mbinguni
Enzi yake kuu.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top