46.Twae Wangu Uzima

Take my life, and let it be

1.
Twae wangu uzima,
Sadaka ya daima;
Twae saa na siku,
Zikutukuze huku.

2.
Twae mikono nayo,
Ifanye upendavyo,
Twae yangu miguu,
Kwa wongozi wako tu.

3.
Twae sauti yangu,
Niimbe kwa Mungu tu;
Itwae na midomo,
Ijae neno lako.

4.
Twae dhanabu pia,
Na yote ya dunia;
Twae yangu hekima,
Upendavyo tumia.

5.
Nia itwae, Mungu,
Haitakuwa yangu;
Twae moyo; ni wako,
Uwe makazi yako.

6.
Twae mapenzi yangu,
Sifa za moyo wangu;
Twae kabisa nafsi
Nniwe wako halisi.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top