Take my life, and let it be
1.
Twae wangu uzima,
Sadaka ya daima;
Twae saa na siku,
Zikutukuze huku.
2.
Twae mikono nayo,
Ifanye upendavyo,
Twae yangu miguu,
Kwa wongozi wako tu.
3.
Twae sauti yangu,
Niimbe kwa Mungu tu;
Itwae na midomo,
Ijae neno lako.
4.
Twae dhanabu pia,
Na yote ya dunia;
Twae yangu hekima,
Upendavyo tumia.
5.
Nia itwae, Mungu,
Haitakuwa yangu;
Twae moyo; ni wako,
Uwe makazi yako.
6.
Twae mapenzi yangu,
Sifa za moyo wangu;
Twae kabisa nafsi
Nniwe wako halisi.