4.Jina La Yesu Salamu!

Jina la Yesu, Salamu!
Lisujudieni,
Ninyi Mbinguni, hukumu
Na enzi mpeni.

Enzi na apewe kwetu,
Watetea dini;
Mkuzeni Bwana wenu,
Na enzi mpeni.

Enyi mbegu ya rehema,
Nanyi msifuni;
Mmeponywa kwa neema,
Na enzi mpeni.

Wenye dhambi kumbukeni
Ya msalabani,
Kwa furaha msifuni,
Na enzi mpeni.

Kila mtu duniani
Msujudieni,
Kote-kote msifuni,
Na enzi mpeni.

Sisi na wao pamoja
Tu mumo sifani,
Milele sifa ni moja,
Ni “Enzi mpeni.”

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top