31.Msingi Imara

Msingi imara, enyi wa kweli,
Umekwisha pigwa kwa neno hili;
Aongeze lipi? Mnayo pia
Kwa Yesu mliomkimbilia.

Wambiwapo vuka maji ya giza,
Mito ya mashaka taipunguza;
Takupa nawe, nikuwezeshe,
Ipata kufaa, isikutishe!

Utakapopishwa ndani ya moto
Nnguvu nitakupa, upate pato;
Huteketezwi, ila taka zako,
Na zitasalia dhahabu zako.

Hata zije mvi, walio wangu
Hawaoni kwisha mapenzi yangu;
Nazo zitakapowenea, ndipo
Mabegani mwangu niwatwekapo.

Na mtu aliyenitegemea
Kamwe kwa adui sitamtia;
Nguvu za jehanam zijapotisha,
Mtu wangu kamwe sitamuacha.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top