29.Baba yetu aliye Mbinguni

I am so glad tha our Father in heaven

1.
Baba yetu aliye Mbinguni
Amenifurahisha yakini
Kuniambia mwake chuoni
Ya kuwa nami Yesu pendoni.

Chorus:
Anipenda Mwokozi Yesu,
Anipenda, anipenda;
Anipenda Mwokozi Yesu,
Anipenda mimi.

2.
Nimuachapo kutanga mbali,
Yeye yu vivyo, hupenda kweli,
Hunirejeza kwake moyoni;
Kweli yu nami Yesu pendoni.

3.
Anipenda! Nami nampenda;
Kwa wokovu alionitenda;
Akanifia Msalabani
Kwa kuwa nami Yesu pendoni.

4.
Haya kujua yanipa raha;
Kumuamini kuna furaha;
Humfukuza mara shetani,
Kwona yu nami Yesu Pendoni.

5.
Sifa ni nyingi asifiwazo,
Moja ni sana katika hizo,
Wala siachi, hata Mbinguni,
Kwimba, “Yu nami Yesu pendoni”.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top