Mungu ni pendo, apenda watu;
Mungu ni pendo, anipenda
Mungu ni pendo, anipenda
Sikilizeni furaha yangu,
Mungu ni pendo, anipenda.
Nilipotea katika dhambi,
Nikawa mtumwa wa shetani.
Akaja Yesu kuniokoa,
Yeye kanipa kuwa huru
Sababu hii namtumikia,
Namsifu yeye siku zote.