17.Namwandama Bwana

1.
Namwandama Bwana kwa alilonena,
Njia yangu huning’azia;
Nikimridhisha atanidumisha
Taamini nitii pia.

Chorus:
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii

2.
Giza sina kwangu wala hata wingu
Yeye mara huviondoa
Woga wasiwasi, sononeko basi.
Huamini nitii pia.

Chorus:
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii

3.
Masumbuko yote, sikitiko lote;
Kwa mapenzi hunilipia,
Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki,
Taamini nitii pia.

Chorus:
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii

4.
Mimi sitajua raha sawasawa
Ila yote yesu kumpa;
Napata fadhili na radhi kamili,
Taamini nitii pia.

Chorus:
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii

5.
Nitamfurahisha na kumtumaini,
Majumbani na njia-njia;
Agizo natenda; nikitumwa hwenda,
Huamini nitii pia

Chorus:
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa yesu, amini ukatii

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top