15.Chakutumaini Sina

Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha
Dhambi zangu kuziosha;

Kwake Yesu nasimma,
Ndiye mwamba: ni salama
Ndiye mwamba: ni salama.

Njia yangu iwe ndefu
Yeye hunipa wokovu;
Mawimbi yakinipiga
Nguvu zake ndiyo nanga.

Damu yake na sadaka
Nategemea daima,
Yote chini yakiisha
Mwokozi atanitosha.

Nikiitwa hukumuni,
Rohoni nina amani
Nikivikwa haki yake
Sina hofu mbele zake.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top