Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha
Dhambi zangu kuziosha;
Sina wema wa kutosha
Dhambi zangu kuziosha;
Kwake Yesu nasimma,
Ndiye mwamba: ni salama
Ndiye mwamba: ni salama.
Njia yangu iwe ndefu
Yeye hunipa wokovu;
Mawimbi yakinipiga
Nguvu zake ndiyo nanga.
Damu yake na sadaka
Nategemea daima,
Yote chini yakiisha
Mwokozi atanitosha.
Nikiitwa hukumuni,
Rohoni nina amani
Nikivikwa haki yake
Sina hofu mbele zake.