Praise Him! Praise Him!
1.
Msifuni, Yesu ndiye Mkombozi,
Imbeni ya pendo zake kuu,
Sujuduni, malaika mlioko,
Jina lake liwe na sifa kuu,
Kama vile mchunga achungavyo.
Vivyo sisi kutwa atuchunga,
Msifuni mlio wake watoto
Msifuni aliye Mchunga.
2 .
Msifuni, Yesu ndiye Mkombozi;
Akateswa tupate ongoka;
Ndiye Mwamba, Dhamana ya kuokoka,
Sujuduni kwake Muangikwa,
Yesu aliyeudhiwa na hamu
Kwa pendo za Baba yake Mungu,
Aliyefyolewa na kusulibiwa,
Msifuni ndilo letu fungu.
Akateswa tupate ongoka;
Ndiye Mwamba, Dhamana ya kuokoka,
Sujuduni kwake Muangikwa,
Yesu aliyeudhiwa na hamu
Kwa pendo za Baba yake Mungu,
Aliyefyolewa na kusulibiwa,
Msifuni ndilo letu fungu.
3.
Msifuni, Yesu ndiye Mkombozi;
Shindukeni, enyi milango juu;
Bwana Yesu tangu milele Mwokozi,
Mvikeni taji, ni yake tu,
Atakuja kuitawala nchi,
Yesu, Mwombezi wetu wa Mungu.
Msifuni, ni mfalme wa salama;
Ndiye kweli Mwana wake Mungu.
Shindukeni, enyi milango juu;
Bwana Yesu tangu milele Mwokozi,
Mvikeni taji, ni yake tu,
Atakuja kuitawala nchi,
Yesu, Mwombezi wetu wa Mungu.
Msifuni, ni mfalme wa salama;
Ndiye kweli Mwana wake Mungu.