114. Bwana Mungu, Nashangaa Kabisa

How Great thou Art

1.
Bwana Mungu nashangaa kabisa
Nikitazama kama vilivyo
Nyota, ngurumo, vitu vingi vyote
Viumbavyo kwa uwezo wako.

Chorus
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu,
Roho yangu na ikuimbie
Jinsi Wewe ulivyo Mkuu.

2.
Nikitembea pote duniani.
Ndege huimba, nawasikia,
Milima hupendeza macho sana,
Upepo nao nafurahia.

3.
Nikikumbuka kama Wewe Mungu
Ulivyompeleka Mwanao
Afe azichukue dhambi zetu,
Kuyatambua ni vigumu mno.

4.
Yesu Mwokozi utakaporudi
Kunichukua kwenda Mbinguni
Nitashukuru na kwimba milele
Wote wajue jinsi ulivyo.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top