111. Neno Lako, Bwana

Lord, thy word abideth

1.
Neno lako Bwana,
Ni imara sana;
Lilo latwongoza,
Lilo latufunza.

2.
Adui wabaya
Wakikaribia,
Neno lake Bwana
Ni ulinzi sana.

3.
Siku za dhoruba
Soma ukiomba;
Neno lake Bwana
Msaada sana.

4.
Ukilamini,
Hwenda na amani;

Chorus
Una na furaha,
Neno ni silaha.

5.
Ni furaha kweli,
Na wingi wa mali,
Neno lake Bwana
Kwa wasiokana.

6.
Neno la rehema,
Tukali wazima;
Faraja ipo papo,
Tufarikanapo.

7.
Tulijue sana
Neno lako, Bwana.
Hapa tukupende,
Kisha kwako twende.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top