I need Thee every hour
1.
Nina haja nawe
Kila saa;
Hawezi mwingine
Kunifaa.
Chorus:
Yesu, nakuhitaji
Vivyo kila saa!
Niwezeshe, Mwokozi,
Nakujia.
2.
Nina haja nawe;
Kaa nami,
Na maonjo haya,
Hayaumi.
3.
Nina haja nawe;
Kila hali,
Maisha ni bure,
Uli mbali.
4.
Nina haja nawe,
Nifundishe
Na ahadi zako
Zifikishe.
5.
Nina haja nawe,
Mweza yote,
Ni wako kabisa
Siku zote.