104. Twasoma ni Njema Sana

There is a better world they say

1.
Twasoma, ni njema sana
Mbinguni, kwa Bwana;
Twasoma dhambi hapana,
Mbinguni, kwa Bwana;
Malaika wema wako,
Vinanda vizuri viko,
Na majumba tele yako,
Mbinguni kwa Bwana.
2.
Siku zote ni mchana,
Ni nchi ya raha;
Wala machozi hapana,
Ni nchi ya raha;
Walioko wauona
Uso wa Mwokozi, tena
Jua jingine hapana,
Ni nchi ya raha.
3.
Nyama na vitu viovu
Havimo kabisa;
Kifo nacho, na ubovu,
Havimo kabisa.
Ni watakatifu wote,
Wameoshwa dhambi zote,
Wasiosafiwa wote
Hawamo kabisa.
4.
Tuna dhambi pia sote,
Mwokozi akafa;
Kwake tutaoshwa zote,
Mwokozi akafa;
Kwake twapata wokovu,
Tutawona utukufu;
Mbinguni tutamsifu;
Mwokozi akafa.
5.
Baba, mama, ndugu zetu,
Twendeni kwa Bwana;
Huku chini iko kwetu,
Twendeni kwa Bwana;
Tusishikwe na dunia,
Na dhambi kutulemea;
Tutupe vya chini pia,
Twendeni kwa Bwana.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top